HOSPITALI YA RUFAA YA MKOA WA TANGA BOMBO KUNUNUA BASI

 

Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhani katika akizungumza wakati wa maadhimisho ya siku ya wauguzi duniani katika Viwanja vya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo kushoto Katibu wa Hospitali hiyo Abdiely Makange na kulia ni Muuguzi Mkuu wa Mkoa wa Tanga Peter Chambo
Meza kuu wakifuatilia matukio mbalimbali katika maadhimiosho hayo
Katibu wa Tana Tawi Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Mwanaisha Nyangasa akisoma risala 
Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhani wa pili kutoka kushoto akiwa na Katibu wa Hospitali hiyo Abdiely Makange wakitembelea mabanda mbalimbali wakati wa maadhimisho hayo
Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhani akizungumza wakati alipotembelea mabanda mbalimbali
Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhani katikati akipata maelezo  wakati alipotembelea mabanda mbalimbali kulia ni Katibu wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Abdiely Makange
Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Juma Ramadhani kulia akiwa na watumishi wa Hospitali hiyo wakati wakiwasha mishumaa walipoingia wodini kwa ajili ya kugawa zawadi na kuwafariji wagonjwa
Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhani kulia akigawa zawadi kwa mgonjwa aliyelazwa kwenye Hospitali hiyo ikiwa ni maadhimisho ya siku ya wauguzu Duniani 
Muuguzi Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Andrew Tusiwe akigawa zawadi kwa wagonjwa katika hospitali hiyo
Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhani akiwa na Katibu wa Hospitali hiyo kulia Abdiely Makange wakielekea kwenye maadhimisho ya siku wa wauguzi baada ya kupokea maandamano

Maandamano ya wauguzi kutoka Kituo cha Toyota kuelekea Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo ikiwa ni kuadhimisha siku ya wauguzi duniani

Wauguzi wakiwa kwenye maandamano hayo

Wauguzi wakianza maandamano ikiwa  ni siku ya maadhimisho ya siku ya wauguzi Duniani
Mkuu wa Idara ya Tehama katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo William Masika akicheza wakati wa maandamano hayo ya siku ya wauguzi duniani yalipopokelewa
Mkuu wa Idara ya Tehama katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo William Masika akicheza wakati wa maandamano hayo ya siku ya wauguzi duniani yalipopokelewa
Sehemu ya wauguzi na wanafunzi wa chuo cha uunguzi wakifuatilia maadhimisho hayo
Sehemu ya wauguzi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo wakifuatilia matukio mbalimbali wakati wa maadhimisho hayo

Kaimu Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo katika aliyesimama akiwa kwenye picha ya pamoja baada ya kumalizika kwa maadhimisho hayo



Na Oscar Assenga,TANGA 

KAIMU Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo Dkt Juma Ramadhani leo amewaongoza wauguzi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa kwenye maaadhimisho ya siku ya Wauguzi Duniani ambapo kilele chake kitafanyika Mei 12 Jijini Mwanzasiku ya wauguzi Duniani. 

Maadhimisho hayo yalianza na maandamano kutoka eneo la Toyota mpaka Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo kulipofanyika kilele cha maadhimisho hayo

Akizungumza wakati wa maadhimisho hayo alisema mipango ya uongozi wa hospitali hiyo kwenye bajeti zijazo na jitihada walizoweka kama taasisi wana mpango wa kununua basi. 

“Kwa sasa Hospitali kwenye bajeti zijazo na jitihada tulizowekeza taasisi wana mpango wa kununua basi kwa ajili ya hospitali  “Alisema Kaimu Mganga Mfawidhi Dkt Juma. 

Awali akisoma risala hiyo Katibu wa Tana Tawi Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Mwanaisha Nyangasa alisema maadhimisho hayo ni kutafakari na kufauta nyayo za mwanzilishi wa huduma za uuguzi na ukunga Bi Florence Night Ngare. 

Alisema wauguzi katika Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Tanga Bombo wamemuenzi kwa kutoa huduma mbalimbali wakati wa maadhimisho hayo ikiwemo za uchunguzi wa saratani ya kizazi na matiti kwa wakina mama ,uchunguzi wa kisukari na macho,shinikizo la damu,kuhamasisha uchangia damu ,upimaji wa VVU kwa hiari na sambamba na utoaji elimu ya afya na lishe kwa wateja mbalimbali 

Aidha alisema pia katika maadhimisho hayo wametoa chanjo za Covid 19 ambapo wananchi waliohudumiwa tokea walipoanza maadhimisho hayo ni 154 ambao walihudumiwa kwa siku moja. 

Hata hivyo alisema kwamba Ukunga ni kada muhimu sana katika kufanikisha utoaji wa huduma nzuri za afya kwenye jamii na unapozungumzia afya bora muuguzi ni sehemu sahihi ya kufanikisha kila mtanzania anakuwa na afya bora. 

Alisema kwamba pamoja hayo kuna mafanikio makubwa ikiwemo mazingira ya kufanyia kazi yameboresha na miundombinu ya hospital na kuwezesha wanafanyakazi kufanya kazi kwenye mazingira mazuri. 

Aidha alisema kwamba pia ni wauguzi kupata nafasi ya kujiendeleza kimasomo,wauguzi kupata motisha mbalimbali,kuongezeka kwa hamasa kwa wauguzi . 

Akizungumzia changamoto wanazokabiliana nayo alisema kwamba changamoto kubwa ni upungufu wa watumishi idara ya ukunga na uuguzi kulingana na mahitaji ya jamii kutokana na kuongezeka kwa vitengo na idara ambazo wauguzi wanahitajika. 

Mwisho.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments