MCHUNGAJI ATANGAZA MUUJIZA WA SIMU KUJICHAJI AUTOMATIC KANISANI


Kushoto ni Mchungaji mtangaza muujiza

Video ya mchungaji mmoja kutoka nchini Nigeria imesambaa mitandaoni akiamuru simu za waumini wake ambazo hazikuwa na chaji, ibada itakapomalizika zitakuwa zimeingia chaji kupitia muujiza, huku muumini mmoja akitoa ushuhuda simu yake ilianza kuchaji ibada tu ilipoanza.

Kupitia videoyako hiyo mtandaoni, mchunga kondoo huyo aliamuru simu ziingie chaji bila kuchomekwa kwenye umeme.

Hivi sasa kumekuwa na wimbi kubwa la wachungaji ambao wamekuwa wakifanya matukio mbalimbali kwa waumini wao wakiita miujiza, ikiwemo kuwanywesha jiki waumini, kuchapisha nguo za ndani zilizo na sura zao, kuwaogesha pamoja na mambo mengine.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments