MWEKA HAZINA WA VICOBA AUAWA KWA KUPIGWA JIWE


Kijana wa miaka 15 (jina linahifadhiwa), mkazi wa Kijiji cha Ngareni, Kata ya Ngoyoni, wilayani Rombo, anashikiliwa na Jeshi la Polisi akidaiwa kumuua mama yake mdogo, Taudensia Massawe (62) kwa kumpasua kichwa akitumia jiwe wakati akikata majani ya ng'ombe.


Tukio hilo linadaiwa kutokea Aprili 24, mwaka huu baada ya kijana huyo kumwambia marehemu akamwonyeshe sehemu ya kukata majani ya ng'ombe na alipofika eneo aliloonyeshwa alimvizia wakati ameinama akikata majani na akampiga na jiwe lililompasua kichwa.


Kijana huyo anadaiwa kufanya mauaji hayo kwa lengo la kupora fedha za Vicoba ambazo mama huyo alikuwa mweka hazina na alikuwa na sanduku la fedha hizo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments