BENKI YA CRDB YASHIRIKI KAMPENI YA KATAA UHALIFU TOA TAARIFA..."USIKAE NA PESA NDANI INACHOCHEA UHALIFU, NJOO BENKI"


Meneja Biashara wa Benki ya CRDB tawi la Shinyanga, Mwanahamisi Iddi akizungumza wakati wa Bonanza la Michezo lililoongozwa na Kampeni ya Kataa Uhalifu Toa Taarifa Shinyanga Bila Uhalifu Inawezekana’ katika kata ya Chibe Manispaa ya Shinyanga.


Na Kadama Malunde - Malunde 1 blog
Benki ya CRDB imeshiriki Bonanza la Michezo lililoongozwa na Kampeni ya Kataa Uhalifu Toa Taarifa Shinyanga Bila Uhalifu Inawezekana’ katika kata ya Chibe Manispaa ya Shinyanga huku ikihamasisha wananchi kuacha tabia ya kuhifadhi pesa ndani ya nyumba kwani vitendo hivyo vinachochea uhalifu.

Kampeni hiyo iliyoandaliwa na Jeshi la Polisi Mkoa wa Shinyanga kwa kushirikiana na wadau mbalimbali kwa Uratibu wa Amos John maarufu MC Mzungu Mweusi imefanyika leo Jumamosi Aprili 15,2023 katika kata ya Chibe kupitia Bonanza la Michezo lililohudhuriwa na mamia ya wananchi ambapo mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa wilaya ya Shinyanga Mhe. Johari Samizi.


Meneja Biashara wa Benki ya CRDB tawi la Shinyanga, Mwanahamisi Iddi amesema Benki ya CRDB inapiga vita masuala ya uhalifu hivyo kuwaomba wananchi kuacha tabia ya kuhifadhi fedha majumbani kwani hicho ni kichocheo cha uhalifu.


"Usikae na pesa ndani ya nyumba kwani kuweka fedha ndani kunachochea uhalifu. Weka pesa zako Benki ili pesa zako ziwe salama lakini pia uwe salama. Njooni Benki ya CRDB mfungue akaunti ili pesa zenu ziwe salama lakini pia tunao mawakala kila mahali. 

CRDB tupo kidijitali zaidi na  tumeongeza wigo kwa wananchi kufanya malipo yao kwa urahisi kupitia SimBanking, SimAccount, Internet banking na CRDB Wakala. karibuni sana",amesema Mwanahamisi.

Meneja Biashara wa Benki ya CRDB tawi la Shinyanga, Mwanahamisi Iddi akizungumza wakati wa Bonanza la Michezo lililoongozwa na Kampeni ya Kataa Uhalifu Toa Taarifa Shinyanga Bila Uhalifu Inawezekana’ katika kata ya Chibe Manispaa ya Shinyanga.
Meneja Biashara wa Benki ya CRDB tawi la Shinyanga, Mwanahamisi Iddi akizungumza wakati wa Bonanza la Michezo lililoongozwa na Kampeni ya Kataa Uhalifu Toa Taarifa Shinyanga Bila Uhalifu Inawezekana’ katika kata ya Chibe Manispaa ya Shinyanga.
Bonanza la michezo likiendelea

Mbio za baiskeli zikiendelea kwenye Bonanza la Michezo likiongozwa na Kampeni ya Kataa Uhalifu Toa Taarifa Shinyanga Bila Uhalifu Inawezekana

Bonanza linaendelea
Mshindi Mbio za baiskeli kundi la wanawake Temineta Charles

Soma pia : 


Tazama Mbio za Baiskeli
Tazama Burudani ya Jeshi la Jadi Sungusungu

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments