MWALIMU ALIYEONEKANA AKIKANYAGA NA KUCHAPA VIBOKO WANAFUNZI ASIMAMISHWA KAZI



Mwalimu akimchapa mwanafunzi


Waziri wa Elimu Prof. Adolf Mkenda amesema kuwa Mwalimu anayeonekana kwenye video fupi inayosambaa mitandaoni akimchapa mwanafunzi kwenye nyayo za miguu yake huku amemkanyaga tayari amekwishachukuliwa hatua za kusimamishwa kazi.


Kwa mujibu wa Waziri wa Maendeleo ya Jamii Dkt. Dorothy Gwajima, amesema Mwalimu huyo ni wa shule ya msingi iliyopo wilayani Kyerwa mkoani Kagera na tukio hilo limetokea Januari 10, 2023.

Aidha waziri Dkt Gwajima akatoa rai kwa Walimu, "Waalimu zingatieni utaratibu wa adhabu kwa wanafunzi, lazima sheria ziheshimiwe,".

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments