AJALI YA COASTER YAUA WATU WATANO


Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani ACP Pius Lutumo.
**
Watu watano wamefariki dunia na wengine 10 kujeruhiwa baada ya basi dogo la abiria aina ya Toyota Coaster kugongana na gari la mizigo aina ya Mitsubishi Canter, katika eneo la Mwavi, Kata ya Kiwangwa wilayani Bagamoyo mkoani Pwani.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Pwani ACP Pius Lutumo, amesema basi hilo dogo la abiria lilikuwa likitoka Bagamoyo kuelekea mkoani Morogoro.

Lutumo amesema kuwa ajali hiyo ilitokea Januari 8 mwaka huu majira ya saa 1:40 asubuhi na kwamba chanzo cha ajali ni basi dogo aina ya Coaster lilikuwa linapita gari lingine bila tahadhari na kugongana na gari lingine kusababisha ajali hiyo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments