BABA AJIUA BAADA YA KUUA MKE, MAMA MKWE NA WATOTO WATANO


Michael Haight mwenye umri wa miaka 42 nchini Marekani amemuua mke wake, mama mkwe na watoto wake 5 na yeye kujiua baada ya mke wake kuwasilisha ombi la talaka jambo ambalo yeye hakulitaka.

Tukio hilo limetokea katika jimbo la Utah nchini Marekani ambapo miili ya watu hao imepatikana ndani ya nyumba ya mashambani katika Jiji la Enoch wakati wa ukaguzi katika boma lao.

Waliofariki ni mke wake Tausha mwenye umri wa miaka 40, mama mkwe wake Gail Earl mwenye umri wa miaka 78 na watoto wake watano pamoja na mhusika huyo Michael Haight.

Polisi wamesema chanzo cha mauaji hayo ni mwaume huyo kutofurahishwa na ombi la talaka lililowasilishwa na mke wake tarehe Desemba 21/2022.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments