MWENYEKITI UMOJA WA VIJANA WA CCM 'UVCCM' AUAWA MADAI YA KUCHEPUKA NA MKE WA MTU



Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama cha Mapinduzi (UVCCM), Ramadhani Hamisi (30) wa Kata ya Kaselya, Iramba mkoani Singida ameuawa kwa kuchomwa na kitu chenye ncha kali tumboni baada ya kudaiwa kukutwa na mke wa Ally Athumani usiku wa Desemba 30, 2022.


Kwa mujibu wa gazeti la Raia Mwema, tukio hilo lililotokea katika Kitongoji cha Msisi linaelezwa kuwa marehemu alikuwa na uhusiano wa kimapenzi na mke wa Athumani, na walishakutwa mara kadhaa wakiwa pamoja na kupewa onyo juu ya tabia hiyo.


Mwenyekiti wa Kijiji cha Kaselya, Wazzael Majja amedai tukio hilo lilitokea majira ya saa nne usiku baada ya mtuhumiwa kuwakuta nyumbani kwake, na ndipo ulipoibuka ugomvi na kuanza kufukuzana gizani kisha kupotezana njiani, lakini mtuhumiwa alimvizia Ramadhani nyumbani bila yeye kujua na kumshambulia.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments