MIILI YA WATU 27 WANAODAIWA KUWA WAHAMIAJI YATUPWA KANDO YA BARABARA



Miili ya watu 27 wanaoaminika kuwa wahamiaji kutoka Ethiopia, "imetupwa" kando ya barabara katika eneo la Ngwerere kaskazini mwa mji mkuu wa Zambia, Lusaka.

Msemaji wa polisi nchini humo Danny Mwale amesema kwamba huenda waliuawa wakiwa katika usafiri.

Manusura mmoja aliyepatikana akipumua kwa shida amekimbizwa katika hospitali ya eneo hilo.


Zambia ni kituo cha usafiri kwa wahamiaji, hasa kutoka Pembe ya Afrika, ambao wanataka kuingia Afrika Kusini.

Bw Mwale alisema wakazi wa Ngwerere walipata miili hiyo leo Jumapili saa 06:00 mchana saa za eneo hilo .Alisema polisi wanaamini wahamiaji hao ni raia wa Ethiopia kulingana na stakabadhi za utambulisho zilizopatikana juu yao.

Miili hiyo imepelekwa katika chumba cha kuhifadhia maiti cha Hospitali ya Ualimu ya Chuo Kikuu cha Zambia.Katika nchi jirani ya Malawi, mamlaka iligundua miili 25 ya wahamiaji wa Ethiopia katika kaburi la pamoja mwezi Oktoba.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments