RAIS SAMIA ATEUA MAKATIBU WAKUU WA WIZARA


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan leo Jumatano Desemba 14, 2022 amefanya uteuzi wa makatibu wakuu wawili wa wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara (Uwekezaji) na Mambo ya Ndani.

Dkt. Samia amemteua Dk Hashil Twaibu Abdallah kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Uwekezaji ambaye awali alikuwa Naibu Katibu mkuu wizara hiyo kwenye upande wa Viwanda na Biashara nafasi ambayo iliyokuwa wazi.


Rais Samia amemteua Kaspar Mmuya kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Ndani ambaye awali alikuwa Naibu Katibu Mkuu Ofisi ya Waziri Mkuu akishughulikia Sera, Bunge na Utaratibu.






Kabla ya Mmuya kuchukua nafasi hiyo, awali Katibu Mkuu wa wizara hiyo alikuwa Christopher Kadio


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553
Previous Post Next Post