KIJANA ANUSURIKA KUUAWA BAADA YA KUNASWA AKIWAFUNDISHA WATOTO USHOGA....AKIRI KUWA NI SHOGA

Jabir Hamisi, mkazi wa mtaa wa Mwatulole, mkoani Geita, amenusurika kuuawa kwa kipigo na mamia ya wananchi, baada ya kukutwa akiwa na kundi la watoto wadogo, akiwafundisha vitendo vya ushoga na ulawiti, hali iliyolazimu Jeshi la Polisi mkoani humo kuingilia kati na kumuondoa katika eneo hilo, ili kunusuru maisha yake.

Akizungumza mara baada ya kukamatwa na wananchi Jabir amesema kitu kilikuwa kinasababisha akiona makundi ya watoto anawaonesha sehemu zake za siri na kuanza kuzichezea, ni kwa sababu tangu afike Geita hajawahi kufanyiwa kitendo hicho ndio maana akajikuta anatumia njia mbalimbali ili aweze kupata watu wa kumfanyia hivyo.


Baadhi ya wananchi waliokuwepo eneo la tukio wamesema kijana huyo alikuwa akifika kwenye makundi ya watoto alikuwa anatoa sehemu zake za siri na kuanza kuzichezea huku akiwahamasisha watoto hao nao wafanye hivyo.


Mwenyekiti wa Polisi jamii Mtaa huo Itanga Timoth amesema walivyomuhoji mtuhumiwa huyo amekiri kwamba yeye ni shoga na vitendo hivyo alivianzia jijini Dar Es Salaam huku mwenyekiti wa mtaa huo Noel Ngasa akiwataka wazazi kuwa walinzi wa kwanza wa watoto wao ili kuwaepusha na vitendo vinavyochochea uharibifu wa maadili.






Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments