BINTI AFARIKI KWA KUPIGWA RADI AKICHUNGA MBUZI


Calista Haule (15) mkazi wa kijiji cha Lifua kata ya Luilo wilayani Ludewa mkoani Njombe amefariki baada ya kupigwa na radi wakati akiwafunga mbuzi chini ya mti baada ya kuwatoa malishoni.

Kwa mujibu wa mashuhuda wa tukio hilo wamesema binti huyo alipigwa na radi hiyo na kufa papo hapo sambamba na mbuzi aliokuwa akiwafunga

Baba wa binti huyo pamoja na dada yake wameelezea masikitiko yao na kudai kuwa binti huyo alirejea nyumbani wiki moja iliyopita akitokea shuleni Mafinga mkoani Iringa kwa ajili ya likizo baada ya shule kufungwa

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments