AMUUA MKEWE KISHA KUMZIKA SHAMBANI BAADA YA KUAMBIWA MTOTO ANAYEMLEA SIYO WAKE

 Mtu mmoja anayefahamika kwa jina Abdallah anatafutwa na Jeshi la Polisi mkoani Pwani kwa tuhuma za kumuua mkewe, Pili Mang’ota (38) mkulima na muuza mbogamboga mkazi wa Sanze, Kata ya Kazimzumbwi wilaya ya Kisarawe.


Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi mkoani humo, Pius Lutumo wakati akizungumza na waandishi wa habari, ameeleza kuwa Abdallah anadaiwa kufanya mauaji hayo baada ya kuambiwa kuwa mtoto wanayemlea si wa kwake.

Kamanda Lutumo amesema tukio hilo lilifanyika Desemba 17 mwaka huu saa nane mchana ambapo marehemu aliaga nyumbani kuwa anaenda kuchuma mboga shambani na hakurudi tena hadi mwili wake ulipokutwa kichakani ukiwa umefukiwa na kuharibika.

“Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na raia wema walifanikiwa kuupata mwili wa marehemu baada ya kufanya msako ambapo alikutwa akiwa amefariki,” ameeleza Kamanda.

Source: ST

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments