BENKI YA CRDB YADHAMINI MKUTANO WA MABALOZI


Waziri wa Mambo ya Nje na Uhusiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Stergomena Tax (kulia) akizungumza na baadhi ya mabalozi walipotembelea banda la Benki ya CRDB katika maonyesho yanayoenda sambamba na Mkutano wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan na Mabalozi, unaofanyika kwenye hoteli ya Velde, Unguja Zanzibar. Kupitia mkutano huo wa kimkakati Benki ya CRDB imeendelea kusisitiza utayari wake katika kusaidia utekelezaji wa diplomasia ya kiuchumi na kuiwezesha Tanzania kunufaika na eneo huru la Biashara Afrika (AfCFTA). Benki ya CRDB ni mmoja wa wadhamini wa mkutano huo ulioanza Novemba 14 hadi 21, 2022.
Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wakubwa Benki ya CRDB, Jacob Nangi (kushoto) akizungumza na Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani, Balozi Abdallah Possi, aliyetembelea banda la Benki ya CRDB katika maonyesho yanayoenda sambamba na Mkutano wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan na Mabalozi, unaofanyika kwenye hoteli ya Velde, Unguja Zanzibar. Benki ya CRDB ni mmoja wa wadhamini wa mkutano huo ulioanza Novemba 14 hadi 21, 2022. Kulia ni Meneja Mwandamizi Uhusiano wa Biashara wa Benki ya CRDB, Lulu Melo.
Balozi wa Tanzania nchini Jamhuri ya Congo, Balozi Said Mshana, akizungumza na Mkuu wa Kitengo cha Wateja Wakubwa Benki ya CRDB, Jacob Nangi wakati alipotembelea banda la Benki ya CRDB katika maonyesho yanayoenda sambamba na Mkutano wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan na Mabalozi, unaofanyika kwenye hoteli ya Velde, Unguja Zanzibar. Benki ya CRDB ni mmoja wa wadhamini wa mkutano huo ulioanza Novemba 14 hadi 21, 2022. Kulia ni Meneja Mwandamizi Uhusiano wa Biashara wa Benki ya CRDB, Lulu Melo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments