WATANZANIA MISS NA MISTER DEAF WAPO TAYARI KWA SHINDANO LA DUNIA LA UTANASHATI NA UREMBO


NA EMMANUEL MBATILO, DAR ES SALAAM

Mchakato wa kumpata Mshindi wa Mashindano ya Wanamitindo na walimbwende wa Dunia umeanza ambao Watanzania wametoa ahadi ya kubakiza ushindi Nyumbani.

Akizungumza kuelekea Shindano hilo ambalo linatarajia kufanyika Oktoba 29,2022 Jijini Dar es Salaam, Mlimbwende Khadija Rajabu amesema wamejipanga ipasavyo licha ya kuwepo kwa changamoto ndogondogo lakini imani yao ni kushinda na kubakisha taji nchini.

Aidha amesema amejipanga vizuri na anaamini ataipeperusha vizuri bendera ya Tanzania katika Mashindano hayo ya dunia.

Kwa upande wa washiriki wengine kutoka mataifa mengine wameipongeza Serikali ya Tanzania kwa kuhakikisha wanaweka mazingira mazuri ambayo yatasaidia kwa kiasi kikubwa mashindano hayo kuwa huru.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments