RAIS SAMIA SULUHU ASALIMIA WANANCHI WA RUNZEWE-GEITA, NYAKANAZI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wananchi wa Runzewe wakati akihitimisha ziara yake Mkoani Geita tarehe 16 Oktoba, 2022.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Waziri wa Nishati January Makamba pamoja na viongozi wengine wakivuta kitambaa kuzindua miradi sita ya umeme, ikiwemo Njia ya kusafirisha umeme wa msongo Kv 220 kutoka Nyakanazi -Geita, Nyakanazi Rusumo, Kituo cha kupokea, kupoza na kusambaza umeme cha Nyakanazi pamoja na njia kubwa za kusafirisha umeme kwenda Mkoa wa Kigoma tarehe 16 Oktoba, 2022 Mkoani Kagera.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akiwa na Waziri wa Nishati January Makamba pamoja na viongozi wengine wakati akikata utepe kuzindua miradi sita ya umeme katika Kituo cha kupokea, kupoza na kusambaza umeme kwenda Mkoani Kigoma na Geita kwenye hafla iliyofanyika Nyakanazi mkoani Kagera 16 Oktoba, 2022

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akitembelea na kukagua miundombinu mbalimbali ya Kituo cha kupokea, kupoza na kusambaza umeme kwenda Mkoani Kigoma na Geita kwenye hafla ya uzinduzi iliyofanyika Nyakanazi mkoani Kagera 16 Oktoba, 2022

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan akizungumza na Wananchi wa Nyakanazi mkoani Kagera wakati akielekea Mkoani Kigoma tarehe 16 Oktoba, 2022

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments