MWENGE WA UHURU ZAZINDUA NA KUWEKA JIWE LA MSINGI MIRADI MANISPAA YA BUKOBA


Na Mbuke Shilagi Kagera.

Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Sahili Geraruma amezindua na kuweka jiwe la msingi katika miradi mbalimbali ya maendeleo katika Manispaa ya Bukoba Mkoani Kagera mara baada ya Mwenge wa Uhuru kupokelewa leo Oktoba 13, 2022 katika maeneo ya uwanja wa shule ya msingi Ibura iliyopo Manispaa ya Bukoba ukitokea Wilaya ya Muleba na kukimbizwa kilometa 27.7 katika Halimashauri ya Manispaa ya Bukoba.


Mbio za Mwenge wa Uhuru zimezindua miradi miwili (2) imeweka jiwe la msingi miradi miwili (2) na kutembelea mradi mmoja (1) ambapo miradi hiyo ni vyumba vya madarasa, mradi wa kikundi cha vijana cha utengenezaji wa thamani, mradi wa ujenzi wa kituo cha Afya Kashai na mradi wa ujenzi wa ujenzi wa tank na upanuzi wa mtandao wa maji ambapo miradi hiyo yote imegharimu kiasi cha zaidi ya bilion nne.


Ikiwa ni kuelekea kilele cha Mbio za Mwenge wa Uhuru ambao Kitaifa utazimwa Mkoani Kagera Manispaa ya Bukoba, Mwenge wa Uhuru utalala katika uwanja wa Mayunga uliopo mtaa wa Uswahilini Kata Bilele Manispaa ya Bukoba na kuzimwa kesho tarehe 14 Octoba 2022 katika uwanja wa Kaitaba na mgeni rasmi atakuwa ni Rais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania Mh. Samia Suluhu Hassan na kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali.
Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Sahili Geraruma pamoja na viongozi mbalimbali akikagua mradi wa ujenzi wa daraja Kyabtembe Manispaa ya Bukoba
Kushoto ni Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Sahili Geraruma akizindua daraja Kyabtembe Manispaa ya Bukoba na kulia ni Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mh. Moses Machali
Kaimu Mkuu wa Wilaya ya Muleba Mh. Kemilembe Rwota akimkabidhi Mwenge wa Uhuru Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mh. Moses Machali katika uwanja wa shule ya msingi Ibura iliyopo Manispaa ya Bukoba
Wa tatu kushoto ni Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mh. Moses Machali akishika Mwenge wa Uhuru katika uwanja wa Mayunga uliopo mtaa wa Uswahilini Kata Bilele Manispaa ya Bukoba
Wa kwanza kushoto ni Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Sahili Geraruma akiweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa kituo cha Afya kashai Manispaa ya Bukoba
Emmanuel Chacha mkimbiza Mbio za Mwenge wa Uhuru Mkoa wa Kagera akiongoza maandamano ya Mbio za Mwenge wa Uhuru kuelekea katika uwanja wa Mayunga uliopo mtaa wa Uswahilini Kata Bilele Manispaa ya Bukoba ambapo utakesha
Wa kwanza kushoto ni Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Sahili Gerarumaakifungua maji kwa ishara ya kumtua mama ndoo kichwani
Katikati ni Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Sahili Geraruma akiweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa madarasa katika shule ya msingi Rwamishenye
Pichani ni Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Sahili Geraruma akiweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa tank na upanuzi wa mtandao wa maji Bugashani Manispaa ya Bukoba
Pichani ni Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mh. Moses Machali na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Sahili Geraruma wakimtua mama ndoo katika mradi wa ujenzi wa tanki na upanuzi wa mtandao wa maji Manispaa ya Bukoba
Pichani ni Mkuu wa Wilaya ya Bukoba Mh. Moses Machali na Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Sahili Geraruma pamoja na wanafunzi wa shule ya msingi Rwamishenye akizindua kilabu ya mapambano dhidi ya rushwa
Wa pili kushoto ni Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Sahili Geraruma akizungumza kabla ya kuweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa tank na upanuzi wa mtandao wa maji Manispaa ya Bukoba
Pichani ni Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa Sahili Geraruma akikata utepe ili kuweka jiwe la msingi katika mradi wa ujenzi wa madarasa katika shule ya msingi Rwamishenye

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments