Tanzia : MBUNGE MUSSA HASSAN MUSSA AFARIKI DUNIA


Mbunge wa Jimbo la Aman (CCM), Mussa Hassan Mussa amefariki dunia leo Alhamisi Oktoba 13, 2022 nyumbani kwake visiwani Zanzibar.

Kupitia taarifa ya kifo hicho iliyotolewa leo Alhamisi Oktoba 13, 2022 na Kitengo cha Mawasiliano na Uhusiano wa Kimataifa, Ofisi ya Spika wa Bunge imeeleza kuwa Spika Dk Tulia Ackson amesema kuwa ofisi ya bunge kwa kushirikiana na familia inaratibu mipango ya mazishi.


“ Nimepokea kwa masikitiko makubwa taarifa ya kifo cha Mhe. Mussa Hassan Mussa, natoa pole kwa familia ya marehemu, ndugu, jamaa, waheshimiwa wabunge na wananchi wa Jimbo la Amani. Mwenyezi Mungu awape moyo wa uvumilivu na subira katika kipindi hiki kigumu”

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments