WAHITIMU TaSUBa WATAKIWA KUTUMIA ELIMU YAO KUSAIDIA JAMII



Katibu Mkuu wa Jimbo Kuu la Kusini mwa Tanzania Kanisa la Waadventista Wasabato Mchungaji Jeremiah Izungu akikabidhi vyeti kwa wahitimu wa Mafunzo ya Muziki TaSUBa ambayo yanaendeshwa na Jimbo Kuu la Kusini Mashariki mwa Tanzania la Kanisa la Waadventista wa Sabato kwenye Mahafali ya Tisa ya Mafunzo ya Muziki TaSUBa yaliyofanyika leo Septemba 10,2022 katika Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa). Katibu Mkuu wa Jimbo Kuu la Kusini mwa Tanzania Kanisa la Waadventista Wasabato Mchungaji Jeremiah Izungu akikabidhi vyeti kwa wahitimu wa Mafunzo ya Muziki TaSUBa ambayo yanaendeshwa na Jimbo Kuu la Kusini Mashariki mwa Tanzania la Kanisa la Waadventista wa Sabato kwenye Mahafali ya Tisa ya Mafunzo ya Muziki TaSUBa yaliyofanyika leo Septemba 10,2022 katika Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa). Katibu Mkuu wa Jimbo Kuu la Kusini mwa Tanzania Kanisa la Waadventista Wasabato Mchungaji Jeremiah Izungu akikabidhi vyeti kwa wahitimu wa Mafunzo ya Muziki TaSUBa ambayo yanaendeshwa na Jimbo Kuu la Kusini Mashariki mwa Tanzania la Kanisa la Waadventista wa Sabato kwenye Mahafali ya Tisa ya Mafunzo ya Muziki TaSUBa yaliyofanyika leo Septemba 10,2022 katika Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa). Katibu Mkuu wa Jimbo Kuu la Kusini mwa Tanzania Kanisa la Waadventista Wasabato Mchungaji Jeremiah Izungu akizungumza katika Mahafali ya Tisa ya Mafunzo ya Muziki TaSUBa ambayo yanaendeshwa na Jimbo Kuu la Kusini Mashariki mwa Tanzania la Kanisa la Waadventista wa Sabato ambayo yamefanyika katika Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa).Mkufunzi Idara ya Muziki TaSUBa, Bw.Heri Kaare akizungumza katika Mahafali ya Tisa ya Mafunzo ya Muziki TaSUBa ambayo yanaendeshwa na Jimbo Kuu la Kusini Mashariki mwa Tanzania la Kanisa la Waadventista wa Sabato ambayo yamefanyika katika Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa).Mwanafunzi wa Mwaka wa tatu Bi.Aksa Nhyenje akisoma risala kwa niaba ya wahitimu wa Mafunzo ya Muziki TaSUBa ambayo yanaendeshwa na Jimbo Kuu la Kusini Mashariki mwa Tanzania la Kanisa la Waadventista wa Sabato leo Septemba 10,2022 katika Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa). Kwaya mbalimbali zikitumbuiza Mahafali ya Tisa ya Mafunzo ya Muziki TaSUBa ambayo yanaendeshwa na Jimbo Kuu la Kusini Mashariki mwa Tanzania la Kanisa la Waadventista wa Sabato leo Septemba 10,2022 katika Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa).

*************

NA EMMANUEL MBATILO, BAGAMOYO

WAHITIMU wa Mafunzo ya Muziki TaSUBa ambayo yanaendeshwa na Jimbo Kuu la Kusini Mashariki mwa Tanzania Kanisa la Waadventista Wasabato wametakiwa kuyaishi yale yote ambayo wamefundishwa na kuwafundisha wengine ili iwe baraka kwa watanzania na watu wote.

Wito huo umetolewa leo Septemba 10,2022 na Katibu Mkuu wa Jimbo Kuu la Kusini mwa Tanzania Kanisa la Waadventista Wasabato Mchungaji Jeremiah Izungu wakati wa Mahafali ya Tisa ya Mafunzo ya Muziki TaSUBa ambayo yanaendeshwa na Jimbo Kuu la Kusini Mashariki mwa Tanzania la Kanisa la Waadventista wa Sabato ambayo yamefanyika katika Taasisi ya Sanaa na Utamaduni Bagamoyo (TaSUBa).

Amesema imekuwa ni muhimu kwa vijana kupata mafunzo hayo kwasababu kumtumikia mungu kunatakiwa akili, maarifa na roho ndo maana wameamua kupeleka kozi eneo hilo ambayo inasaidia waimbaji wao kumuimbia mungu kwa maana ya kumtukuza kwasababu ni wajibu kufanya hivyo.

"Nyimbo ni ibada lakini pia namna ya kufanya amani katika mioyo ya watu ni hubiri ni mafundisho ambayo ni muhimu sana kwa watanzania kwa ujumla na hapa ujumbe ambao nimeuleta nikuwataka washiriki wa kanisa na watanzania kupenda nyimbo za ibada". Amesema Mchungaji Izungu.

Aidha amewataka watanzania kuwa na umuhimu wa kupenda maandiko matakatifu na kuyasoma, kuyasikia, kuyaishi na kuyafundisha kama nyenzo ya kufanya amani idumu kuwepo ulimwenguni kote.

Nae Mkufunzi Idara ya Muziki TaSUBa, Bw.Heri Kaare amesema wamekuwa na programu za muda mfupi kwa kanisa la waadventista wasabato ambapo ili mtu aonekane amehitimu haya mafunzo anapaswa kuja awamu tatu, kwahiyo wapo walikuja kwa awamu ya kwanza, ya pili na yatatu.

Amesema tangu waanze mpaka sasa mabadiliko ni makubwa, wengi wanafika wakiwa hawajui chochote kuhusu muziki lakini wanaondoka wanaweza kusoma muziki kwenye karatasi ama kwenye vitabu pamoja na kupiga ara za muziki.

"Watu wote ambao wanatamani kuja kujifunza muziki waje, muziki ni taalumu kwa maana lazima uingie darasani uweze kunolewa". Amesema

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments