MGAMBO ACHOMWA KISU AKIAMUA UGOMVI WA MKE NA MME POLISI


Kisu

Askari mgambo Fred William (47), mkazi wa Kijiji cha Mkengwa, Rorya mkoani Mara, amefariki dunia baada ya kuchomwa na kisu shingoni akiwa katika kituo cha polisi Mkengwa, wakati akimzuia aliyemchoma kisu kutomfanyia fujo mke wake aliyekimbilia kituoni hapo kuomba msaada.


Tukio hilo limetokea Agosti 30, 2022, ambapo marehemu alikuwa akimzuia mtuhumiwa kutomfanyia fujo mke wake aliyekimbilia kituoni hapo kuomba msaada kutokana na kwamba walikuwa na ugomvi na alikuwa akitaka kumuua.

Mashuhuda wa tukio hilo wamesema marehemu alichukua jukumu hulo kutokana na kwamba Askari Polisi wa kituo hicho walishindwa kumdhibiti mtuhumiwa kwani hawakuwa na silaha ya aina yoyote.

Chanzo - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments