ASKOFU MACHIMU AMPONGEZA RAIS SAMIA KUTOA RUZUKU YA MBOLEA KWA WAKULIMA

Askofu Raphael Machimu akiwasihi waumini kuliombea Taifa la Tanzania na kumpongeza Rais Samia Suluhu Hassan kutoa ruzuku ya mbolea kwa wakulima.
Askofu Raphael Machimu akizungumza kanisani


Askofu wa Kanisa la EAGT Ushirika Makimbilio Healing Center mjini Shinyanga, Raphael Machimu amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kutoa ruzuku ya mbolea.


Askofu Machimu amesema hayo leo Ijumaa Septemba 2,2022 wakati wa ibada iliyoambatana na zoezi la kuhitimisha kongamano la kurugenzi ya kusifu na kuabudu kongamano lililohusisha zaidi ya vijana elfu moja kutoka katika Kanda za maziwa makuu inayojumuisha mikoa nane ya Kigoma ,Kagera,Geita,Mwanza,Simiyu ,Shinyanga ,Mara na Tabora.


Amesema ni vyema wananchi wakawekeza katika sekta ya kilimo hali itakayowawezesha kunufaika na ruzuku ya mbolea iliyotolewa na serikali.


Askofu Machimu amesema ni wajibu wa waumini wa kanisa hilo na madhehebu mengine kuedelea kusali na kuomba katika familia zao wakiliombea Taifa na viongozi wake maana pasipo amani na utulivu waumini hawawezi kupata nafasi ya kufanya shughuli zao ikiwemo kusifu na kuabudu.


Aidha Askofu Machimu amempongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan kwa kuendelea kutoa uhuru wa kuabudu hali inayo wapa viongozi wadini kufanya kazi ya kulitangaza neno la Mungu kwa uhuru.


“Tunaishukuru serikali kwa kuendelea kudumisha amani ya nchi na kuya ruhusu madhehebu mbalimbali kufanya shughuli zake kwa uhuru maana kuna baadhi ya nchi zinazo kosa uhuru huo”,amesema Askofu Machimu.


Pia Machimu, amewashukuru waimbaji kwa kuendelea kuhubiri na kulitangaza neno la mungu kwa njia ya nyimbo huku akiwasii waimbaji kuyaishi yale wanayo imba katika nyimbo zao.


Naye mkurugenzi wa Idara ya kusifu na kuabudu Taifa kutoka Nyanda za juu kusini jimbo la Mbalari mch. Gidion Malatila amebainisha kuwa katika kongamano hilo wamewasii waimbaji kutenda matendo yanayo mpendeza mwenyezi Mungu wakati wa utume wao.


Kwa upande wao badhi ya waimbaji walio hudhuria kongamano hilo lililo dumu kwa mda wa siku tano wameahidi kuyazingatia maagizo na ushauri uliotolewa na Askofu kwa kuyaishi yale wanayo imba katika nyumba za ibada ikiwemo kuendelea kuomba na kusali wakiliombea Taifa la Tanzania na viongozi wake.
Viongozi wakiendelea kusifu na kuabudu.
Viongozi wa kurugenzi wa idara ya kusifu na kuabudu kanda za maziwa makuu.
Mkurugenzi wa idara ya kusifu na kuabudu taifa kutoka nyanda za juu kusini jimbo la Mbalali Mch. Gidion Malatila.
Wanakwaya wakisifu kwenye kongamano hilo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments