JAMAA AKATA NYETI ZAKE AKIOTA ANACHINJA MBUZI

Mwanaume mmoja nchini Nigeria mwenye umri wa miaka 42 anapambania kuokoa maisha yake baada ya kuzikata sehemu zake za siri na kisu ndotoni, baada ya kuota anachinja mbuzi kwa ajili ya kumsaidia mke wake kuandaa chakula cha jioni.


Tukio hilo limetokea Agosti 12, 2022, na kusema kwamba baadaye alikuja kushtuka na kugundua kwamba alikuwa akizikata sehemu zake za siri badala ya mbuzi kama alivyokuwa anaota.

Imeelezwa kwamba mke wa mwanaume huyo hakuwepo nyumbani na ndipo alipopigiwa simu na majirani zake kumuarifu kwamba mume wake amejeruhiwa na ndipo alipowahi kurudi nyumbani na kumkuta amezishikilia sehemu zake za siri na kisha kumpeleka hospitali.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments