ATUPWA JELA MIAKA 4 KWA KUMCHAPA VIBOKO KARANI WA SENSA




Amos Nyang'waji

Kijana mmoja aliyefahamika kwa jina la Amos Nyang'waji (25), mkazi wa Kijiji cha Matui wilayani Kiteto mkoani Manyara, amehukumiwa kwenda jela miaka minne kwa kosa la kumcharaza viboko Karani wa Sensa na kuharibu kishikwambi chake wakati akitekeleza majukumu yake.


Hukumu hiyo imetolewa katika Mahakama ya Hakimu Mkazi wilaya ya Kiteto, na Hakimu Mosi Sasy, ambapo awali akisoma mashtaka hayo, Mwendesha Mashtaka ya Polisi Joseph Kijo, amesema Agosti 25, 2022, katika Kijiji hicho cha Matui wilayani Kiteto mtuhumiwa Amosi Nyang'wali akiwa nyumbani kwa kaka yake alimpiga Karani wa Sensa aliyefahamika kwa jina la Cecilia Paulo.

Alipotakiwa kujitetea mtuhumiwa huyo alisema yeye ana tatizo la akili lililomfanya atende kosa hilo ambapo Hakimu Sasy alisema, kwa kawaida kosa la kwanza la shambulio la mwili anapaswa kwenda jela miaka mitano na kosa la pili la kuharibu mali ni jela miaka saba lakini baada ya kuiomba Mahakama impunguzie adhabu aliamriwa kwenda jela miaka 4 na faini laki 7 na fidia laki 5

Hakimu Sasy amesema adhabu hiyo iwe fundisho kwa wengine wenye tabia ya kukwamisha kazi za serikali na hata kuharibu mali ya serikali ambayo inatumia kodi ya wananchi kuwahudumia.

CHANZO - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments