SIMBA WASAJILI BEKI MPYA



Beki mpya wa Simba Mohamed Ouattara

KLABU ya Simba imekamilisha usajili wa mlinzi wa kati kutoka klabu ya Al Hilal ya nchini Sudan Mohamed Ouattara.

Ouattara amesaini kandarasi ya miaka miwili kuwatumikia wekundu wa msimbazi na anaingia moja kwa moja kuziba pengo la Pascal Wawa aliyemaliza mkataba wake na tayari ameshatimka klabuni hapo.


Ouattara ametambulishwa rasmi kupitia ukurasa wa klabu hiyo wa mtandao wa kijamii wa Instagram.


Beki huyo raia wa Ivory Coast mwenye umri wa miaka 29 amewahi pia kukipiga katika Ligi Kuu nchini Morocco akiwa na moja ya miamba ya soka Barani Afrika Klabu ya Wydad Casablanca.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments