MFANYAKAZI WA BENKI YA NMB APOTEZA WATOTO WAWILI AJALI YA BASI LA SHULE


Simon Jogwe Mfanyakazi wa NMB aliyepoteza watoto wawili kwa mpigo katika ajali ya gari la King David

MFANYAKAZI wa Benki ya NMB Mkoani Mtwara, Simon Jogwe ni miongoni mwa wazazi waliopoteza watoto katika ajali ya gari iliyotokea leo Kata ya Magegeni, Manispaa ya Mtwara Mikindani.


Jogwe amepoteza watoto wa pekee wawili Johari Simon miaka 7 na Emmanuel Simon miaka 5, ambao wote walikuwa ni wanafunzi wa shule ya msingi King David.


Ajali hiyo iliyohusisha gari la shule hiyo (King David Primary School) imeua watu 10, wakiwemo wanafunzi nane, dereva na mama mmoja ambaye aliomba lift katika gari hiyo.


Kwa mujibu taarifa ya Mganga Mkuu wa Mkoa Dk. Hamad Nyembea, wanafunzi watano wasichana na watatu wavulana ndiyo waliopoteza maisha.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments