SIMBA SC YAIBUKA NA SLOGAN MPYA "WE ARE UNSTOPPABLE".....HATUSHIKIKI HATUZUILIKI


CEO wa Simba Barbara Gonzalez Kushoto akizindua Slogan mpya kwa msimu huu We Are Unstoppable (Kushoto) ni malkia wa Bongo Fleva Zuchu
 **
Mtendaji Mkuu wa Simba Barbara Gonzalez amesema kuwa msimu huu klabu hiyo imejipanga kurudisha makombe yote ya ndani na kuhakikisha inafika nusu fainali ya ligi ya Mabingwa Afrika.


Barbara ameyasema hayo leo kwenye uzinduzi wa Simba Week uliofanyika Mbagala Zakheim Dar es salaam ambapo pia ameongeza kuwa usajili bado unaendelea na kuanzia wiki ijayo wataendelea kushusha wachezaji wengine.


“Safari hii hakuna kuteleza tena. Tumejipanga kuhakikisha tunarudisha mataji yote kuanzia Ligi Kuu, FA na kufika Nusu Fainali ya Klabu Bingwa Afrika”


Kuelekea kilele cha Simba Day ambayo itafanyika Agosti 8, 2022 Simba imezindua Slogan Mpya We Are Unstoppable Hatushikiki Hatuzuiliki.

Msimu uliopita Simba ilizisiwa ujanja na watani zao Yanga baada ya kuzoa makombe yote ikiwemo la ligi kuu ya Nbc, pamoja na Kombe la shirikisho la Azam (Azam Sports Federation Cup) na Ngao ya Jamii.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments