BINGWA WA MAJI ACHAKAZWA SHINYANGA


Anasifika kwa kumwagia maji marafiki zake pale wanapoadhimisha siku zao za kuzaliwa ‘ Birthday’..Kama una birthday usiombe ukutane naye... Si mwingine ni Mwandishi wa habari maarufu Josephine Charles ambaye hivi karibuni amezindua Kola Online Tv na Kola Liquid Soap…Josephine aliyebatizwa kuwa Mkuu wa Kitengo cha maji , Humlazimu kutumia mbinu zote ili kuhakikisha anatimiza lengo lake la kumwagia maji ndugu na marafiki.. Na hufurahia sana kwa kitendo hicho!!

Sasa leo Jumamosi Julai 23,2022 akiwa anatimiza miaka kadhaa tangu kuzaliwa kwake..Mrembo huyo anayejulikana kwa jina la Josephine Charles mkazi wa Shinyanga amejikuta katika wakati mgumu baada ya kunaswa na wadau kisha kupigwa maji na matope ya kutosha kama anavyoonekana kwenye picha!!

La haula!! Josephine Charles yule Bingwa wa maji, mbabe wa maji ya Birthday hana ujanja leo, ama kweli malipo ni hapa hapa duniani.

Happy Birthday Josephine Charles!!
Josephine Charles alivyoanza kumwagiwa maji na marafiki zake
Josephine Charles akiendelea kuoga maji na matope

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments