AJALI YA GARI MCHOMOKO YAUA WATU WATANO SIMIYU.

 

Watu watano wamefariki dunia na wengine 11 wamejeruhiwa katika ajali ya gari iliyotokea eneo la Magereza nje kidogo ya mji wa Bariadi Wilaya ya Bariadi mkoani Simiyu usiku wa kuamkia leo Julai 13, 2022.


Kamanda wa Polisi Mkoa Simiyu, Blasius Chatanda amesema kuwa ajali hiyo imehusisha magari madogo ya abiria.

"Nimefika eneo la ajali nimeona waliofariki wote ni wanaume. Gari moja mchomoko lilikuwa likitokea Lamadi na lingine Bariadi. Dereva aliyekuwa akitoka Lamadi aliova-take ndipo akakutana na mwenzake. Chanzo ni mwendo kasi. Madereva wamejeruhiwa na wapo chini ya ulinzi,"amesema

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments