DIAMOND PLATNUMZ ATHIBITISHA KUNUNUA NDEGE


Diamond Platnumz akitumbuiza Jijini Berlin Ujerumani

KAMA ulikuwa unadhani ni stori stori tu za mtandaoni, habari ikufikie Nasibu Abdul ‘Diamond Platnumz’ amethibitisha kununua ndege.


Ndio, kwa kinywa chake Diamond ametamka akiwa nchini Ujerumani akiwa ameshika kipaza sauti cha chombo cha habari cha kimataifa cha DW nchini Ujerumani.
Diamond alikuwa akizungumzia namna msanii unatakiwa kuishi au kuwa ili kupata ile heshima unayostahili na kuingiza mkwanja wa kutosha (msanii unavyotakiwa kujiwekeza mwenyewe).


“Mfano kwa mtu kama mimi ambaye nimetokea mtaani, kwa sasa nanunua gari la kifahari lenye thamani hadi tsh. bilioni 2.3…kwa hiyo itabidi ufanye hivyo kwani usipofanya hivyo hawatakuona wewe ni wa thamani (watakuchukulia poa)… na sasa tayari nimeshanunua ndege binafsi (private jet),” Diamond Platnumz.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments