KONGAMANO LA AIESEC LAFANYIKA CHUO KIKUU CHA MZUMBE


Afisa mwajiri wa kampuni ya Barrick, Alfa Rashid (kushoto) akibadilishana mawazo na Watendaji kutoka taasisi ya AIESEC.
****
Kongamano la kuwajengea Wanafunzi wa vyuo vikuu lililoandaliwa na taasisi ya AIESEC tawi la Tanzania na kudhaminiwa na Kampuni ya Madini ya Barrick, kwa kushirikiana na wadau mbalimbali limefanyika katika Chuo Kikuu cha Mzumbe –Morogoro, ambapo wataalamu mbalimbali walitoa mada za kuwajengea uwezo Wanafunzi kusoma kwa bidii na kuzidi kuwa wabunifu ili waweze kwenda sambamba na mabadiliko ya kiteknolojia na kidigitali ili waweze kunufaika na fursa mbalimbali zinazojitokeza na kuwa na uwezo wa kujiajiri.
Baadhi ya Wanafunzi wa Chuo Kikuu cha Mzumbe,kampasi ya Morogoro wakifuatilia mada wakati wa kongamano hilo.
Mhadhiri wa Chuo kikuu Mzumbe Dkt. Albogasti Mkabila, akibadilishana mawazo na Diwani wa kata ya Mzumbe, Godfrey Fransis, wakati wa kongamano.
Baadhi ya Wanafunzi wakipiga picha ya pamoja na watoa mada,waandaaji na wawakilishi wa makampuni yaliyofadhili kongamano hilo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments