JINAMIZI LA SARE LAENDELEA KUITESA SIMBA SC



**************************

NA EMMANUEL MBATILO

KLABU ya Simba Sc imelazimisha sare ya 2-2 dhidi ya timu ya Namungo Fc mchezo wa ligi ambao ulipigwa kwenye dimba la Ilulu Mkoani Lindi.

Namungo ilianza kupata bao kupitia kwa kiungo wao Jacob Masawe ambaye alipachika bao kali baada ya kupigwa kona na Shiza Kichuya na kumalizia nyavuni.

Simba Sc iliandelea kutafuta bao lavkusawazisha kwa kujaribu kutengeneza nafasi nyingi lakini baadae walibahatika kusawazisha bao kupitia kwa Shomari Kapombe.

Mechi mpaka mapumziko matokeo yalikuwa 1-1 kabla ya Obrey Chirwa kuoachika bao la kuongoza kwa timu yake na baadae dakika za lala salama Simba Sc kusawazisha kupitia kwa Kibu Dennis.

Mchezaji wa Namungo Fc, Hashimu Manyanya alipewa kadi nyekundu mara baada ya kuoneshwa kadi za njani mbili kwa utovu wa nidhamu.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments