HILI NDIYO GARI LENYE GHARAMA ZAIDI DUNIANI


Mercedes-Benz 300 SLR ‘Uhlenhaut Coupe’

Kampuni ya Mercedes-Benz siku ya jana iliweka rekodi ya kuuza gari la gharama zaidi Duniani, kwa kuuza gari lake aina ya Mercedes-Benz 300 SLR ‘Uhlenhaut Coupe’ ya mwaka 1955 kwa kiasi cha dola milioni 142 sawa na Tsh bilioni 330.


Kabla ya hapo gari aina ya Ferrari 250 GTO ya mwaka 1963 ndiyo lilikuwa gari la gharama zaidi, mwaka 2018 liliuzwa kwa kiasi cha dola milioni 70 sawa na Tsh bilioni 163.

Pesa zilizopatikana katika mauzo ya gari hii zitatumika kuanzisha mfuko wa Mercedes Benz kwa ajili kusaidia ya wanafunzi katika masomo ulimwenguni.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments