MAMA AJIFUNGUA MTOTO MWENYE VICHWA VIWILI

Wanandoa kutoka eneo la Emoloi, Teso Kusini, katika Kaunti ya Busia nchini Kenya wanafadhaika baada ya mama kujifungua mtoto mwenye vichwa viwili.

Mama huyo, Nancy Apoma mwenye umri wa miaka 25, ambaye ni mama wa watoto wawili, anasema alijifungua mtoto huyo katika Hospitali ya Alupe.

 Punde alijifungua, aligundua kuwa mtoto huyo alikuwa na uvimbe mkubwa lakini kutokana na kukosa fedha aliruhusiwa kuenda nyumbani bila kujua kiini cha ugonjwa huo.

“Nilijifungua mtoto Given Aramisi katika Hospitali ya Alupe wiki tatu zilizopita. Mtoto wangu ana vichwa ‘viwili’ na aliruhusiwa kuondoka hospitalini kabla ya mtu yeyote kunieleza tatizo, sababu yake na tiba yake,” alisema.

Apoma alisema kipindi chote cha ujauzito wake, hakuwa na matatizo yoyote na alikuwa akienda kliniki kila mwezi. “Ultrasounds zilifanywa na walinihakikishia kuwa mtoto yuko katika hali ya kawaida na yuko katika hali nzuri zaidi ya kunipa dawa na vidonge vya madini ya chuma, ambavyo nilikuwa natumia. Kwa kweli sijui jinsi hii ilifanyika," alieleza 

Daktari wake anasema nini?

Kulingana na Brian Matsiza, afisa wa matibabu katika Hospitali ya Alupe mama huyo hakuwa na matatizo wakati wa kujifungua. "Alijifungua kawaida, lakini kwa bahati mbaya mtoto alikuwa na ulemavu wa kuzaliwa na katika kisai hiki, ndio tunayoita kama kasoro za neural tube na hutokea mwezi wa kwanza wa ujauzito. Huu ni tatizo la ubongo na lenyewe ilifunikwa na hivyo hatukuwa na wasiwasi na maambukizi," alisema Matsiza.

Kasoro za kufungwa kwa mirija ya neva mara nyingi zinaweza kutambuliwa wakati wa ujauzito kwa vipimo mbalimbali vya kimwili na kemikali. Kutokana na Hospitali ya Alupe kukosa vifaa vya kufanya upasuaji unaohitajika, Matsiza alisema waliagiza wanandoa hao kwenda Hospitali ya Mafunzo na Rufaa ya Moi.

Lakini wanandoa hao wanasema hawana uwezo wa kulipia upasuaji huo. "Hatuna kazi na tunataabika sana na hatuna chochote cha kumpa mtoto wetu matibabu anayohitaji," Apoma alisema, akiwaomba wataalam wa matibabu, serikali na Wakenya msaada.


Alisema kuwa mume wake Steven Okoromong, 27, amekaa kimya bila msaada.

CHANZO - Tuko News

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments