WAZIRI WA MAJI JUMAA AWESO ATINGA BUNGENI NA WAKE ZAKE WAWILI.....'HAYA NI MAHABA MAZITO SANA'


Waziri wa Maji Jumaa Aweso, akiwa na wake zake
**
Waziri wa Maji Jumaa Aweso, amesema kwamba ushirikiano anaopewa na wake zake wawili hauoneshi tu kama ni mapenzi bali ni mahaba mazito na kwamba hata kuchakarika kwake kunatokana na ukaribu wao kwake.

Kauli hiyo ameitoa hii leo Mei 12, 2022, Bungeni Dodoma, wakati akiwasilisha bajeti ya wizara hiyo kwa mwaka wa fedha 2022/2021, ambapo wake zake wote wawili wamehudhuria bungeni kumshuhudia.

"Leo wake zangu wote wawili wamekuja hapa kuni-support haya sio mapenzi haya ni mahaba mazito sana, mimi ninawapenda sana ukiniona nachakarika ni kwa sababu ya ukaribu wao na ushirikiano mkubwa wanaonipa, mimi Jumaa Aweso nitaendelea kuwapenda sana wake wangu," amesema Waziri Aweso.

Chanzo - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments