CHAMA CHA WANASHERIA WANAWAKE TAWLA CHAFANYA MKUTANO MKUU WA MWAKA DAR


Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Chama cha Wanasheria Wanawake Tanzania (TAWLA) Bi. Lulu Ng'wanakilala  akifungua mkutano Mkuu wa 32 wa Mwaka wa Chama hicho unaofanyika kwenye hoteli ya Slipway jijini Dar es Salaam ambapo wanasheria mbalimbali wananwake ambao ni wanachama wa chama hicho wanashiriki. Picha na John Bukuku
Mkurugenzi Mtendaji wa Chama cha Wanasheria Wanawake (TAWLA) Bi. Tike Mwambipile akitoa maelezo kwenye mkutano huo kabla ya kumkaribisha Bi. Lulu Ng'wanakilala Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya (TAWLA) ili kuzungumza.
 Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya (TAWLA) Bi. Lulu Ng'wanakilala  na Jaji Mstaafu Joaquine De- Melo wakiwa katika mkutano huo.
Dr. Hellen Kijo Bisimba akitoa mada katika mkutano huo unaofanyika kwenye hoteli ya Slipway jijini Dar es Salaam.
Jaji Mstaafu Joaquine De- Melo ambaye ni mwanachama wa (TAWLA) akitoa nasaha zake kwa wanachama katika mkutano huo.
Dr.  Gavin Kweka mwanasaikilojia akizungumza na wananchama wa (TAWLA) na kuwapa mada mbalimbali kuhusu msongo wa mawazo unavyoathiri watu wengi katika maisha.
Picha mbalimbali zikiwaonesha wanasheria wanawake ambao ni wanachama wa TAWLA wakifuatilia hoja mbalimbali katika mkutano huo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments