RAIS SAMIA AWATAKA WATUMISHI WA UMMA KUACHA KUWA NA HESHIMA YA UOGA



Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan
**
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan amewataka viongozi na watumishi wa umma kuwa na heshima ya kweli kutoka ndani ya mioyo yao na kila mtu kutimiza majukumu yake kwa maadili na weledi mkubwa kwa maslahi mapana ya taifa.

Rais Samia ameyasema hayo leo jijini Dodoma wakati akiwaapisha viongozi mbalimbali walioteuliwa hivi karibuni ikiwa pamoja na mawaziri waliobadilishwa kutoka wizara moja kwenda nyingine.

Katika hotuba yake Rais Samia ameabainisha kuwa licha ya serikali ya awamu ya tano kusifiwa kwa kukuza heshima kwa watumishi wa umma, lakini heshima hiyo ilikuwa ya woga, na hivyo akawataka watumishi kuwa na nidhamu kutoka ndani ya mioyo yao.

“Tunasifiwa kuwa awamu ya tano tulikuza heshima kwa watumishi wa umma, heshima iliyokuzwa ni heshima ya woga kwa sababu alikuwepo simba wa Yuda, ambaye ukimgusa sharubu anakurarua, heshima inayotakiwa iwe ya moyoni” ,amesema Rais Samia Suluhu Hassan

Aidha Rais Samia akasisitiza kuwa ataendelea kufanya kazi kwa kalamu, na kamwe hawezi kuwafokea watendaji walio chini.

Chanzo - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments