TAARIFA YA ULIPO MSIBA WA MSANII MAUNDA ZORRO


Msanii Maunda Zorro enzi za uhai wake

Mwimbaji wa Bongofleva, Maunda Zorro amefariki dunia usiku wa kuamkia leo Aprili 14, 2022. Chanzo cha kifo chake ni ajali ya gari.

Ndugu wa damu wa Maunda Zorro msanii wa Bongofleva Banana Zorro amethibitisha kutokea kwa msiba wa mdogo wake.

Msanii Banana Zorro ametoa taarifa ya kinachondelea kwenye msiba wa dada yake Maunda Zorro kwa kueleza kwamba kwa sasa msiba upo Maweni Kigamboni kwa Mzee Zorro na taarifa zaidi kuhusu msiba huo zitatolewa baadaye.

Taarifa ya Maunda Zorro kufariki dunia zimetoka usiku wa kuamkia leo huku chanzo cha kifo chake ni ajali ya gari iliyotokea Kigamboni Dar es Salaam.



Picha ya aliyekuwa msanii Maunda Zorro


Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments