Dkt. FIMBO : MTUMIAJI WA DAWA ZA KUONGEZA NGUVU ZA KIUME ATAKUFA


Mkurugenzi Mkuu wa Mamlaka ya Dawa na Vifaa Tiba (TMDA) Dkt. Adam Fimbo
**
Mkurugenzi Mkuu wa TMDA Dkt. Adam Fimbo, amesema kwamba watumiaji wa dawa za kuongeza nguvu za kiume wapo kwenye hatari zaidi ya kupoteza maisha kwa sababu dawa hizo hupanua mishipa ya damu.

Dkt. Fimbo, amesema kwamba dawa za kuongeza nguvu za kiume zinaongoza kwa sasa kwa kununuliwa zaidi kwenye maduka makubwa ya dawa nchini.

"Watumiaji wa dawa hizi watakufa kwa sababu zinapanua mishipa ya damu, mishipa ya kichwani ikishapanuka, itapasuka na hivyo mtumiaji wa dawa hizi atakufa tu,"amesema Dkt. Fimbo.

Chanzo - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments