WASIOJULIKANA WAUA NA KUIBA MAFUTA YA KULA



Polisi katika eneo la Uranga kaunti ya Siaya nchini Kenya, wanachunguza mauaji ya kijana mmoja mwenye umri wa miaka 19, baada ya watu wasiojulikana kumvamia dukani na kumuua kisha kuondoka na mafuta ya kula.

Tukio hilo limetokea Jumatano, Aprili 13, 2022, ambapo kwa mujibu wa polisi wameeleza kwamba mwili wa kijana huyo uliokuwa umekatwakatwa vibaya, ulipatikana kando ya barabara, karibu na duka hilo, siku tatu baada ya kuripotiwa kutoweka.

Taarifa zimeeleza kwamba kijana huyo alikuwa amemaliza mtihani wake wa kidato cha nne (KCSE) 2021, akisubiri matokeo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments