WATU WANNE WAFARIKI, 37 WAJERUHIWA AJALI GARI KUGONGA WATEMBEA KWA MIGUU TANGA



Watu wanne wamefariki dunia na wengine 37 kujeruhiwa katika ajali iliyohusisha magari mawili wilayani Handeni mkoani Tanga.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga (RPC), Safia Jongo amethibitisha kutokea kwa ajali hiyo ambayo ilitokea usiku wa kuamkia leo Jumatano Machi 16, 2022 katika Kijiji cha Sindeni.

Kamanda Jongo amesema kuwa basi ndogo la abiria aina ya Coaster iligonga Toyota Hiace na watembea kwa miguu na kusababisha vifo vya watu wanne na majeruhi 37.

"Chanzo cha ajali hii ni gari aina ya Isuzu Jorney ikitokea Tanga mjini kwenda Handeni, iligonga watembea kwa miguu na gari ambayo iliharibika njiani ambapo watu watatu walifariki hapohapo na mmoja alifariki hospitali akiwa anapatiwa matibabu huku saba wakijeruhiwa sana na wengine wamepata michubuko " amesema

Mganga mkuu Hospitali ya mji Handeni, Dkt Hudi Shehdadi amesema kuwa walipokewa majeruhi 38 ambapo mmoja alifariki dunia akiwa bado anapatiwa matibabu.


Chanzo : Mwananchi

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments