MUHIMBILI YATOA UFAFANUZI VIDEO YA PROF. JAY INAYOSAMBAA MTANDAONI



Hospitali ya Taifa Muhimbili leo Machi 10, 2022 imetolea ufafanuzi taarifa inayosambaa kwenye mtandao wa kijamii kuhusu Joseph Haule maaruru Professor Jay na kusema “Kuna video inayosambazwa na Mtandao ikimuonesha Profesa Jay akipatiwa matibabu Muhimbili Hospitali Upanga”.

“Uongozi wa Hospitali unatoa taarifa kuwa video hii haijarekodiwa na kusambazwa na Hospitali, tumesikitishwa na tunalaani vikali kitendo hiki cha kumrekodi mgonjwa anayepigania uhai wake ICU na kuisambaza, hiki ni kiwango cha juu cha kukosa utu na maadili”.

“Tunafuatilia kwa ukaribu tukio hili ili kubaini chanzo cha video hiyo ili hatua stahiki zichukuliwe, Wananchi endeleeni kuwa na imani na Hospitali ta Muhimbili” imeeleza taarifa iliyotolewa na Hospitali ya Muhimbili.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments