MWILI WA Dkt. MWELE MALECELA WAAGWA KARIMJEE


Rais wa Zanzibar, Dk. Hussein Mwinyi na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa pamoja na Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson wameongoza waombolezaji viwanja vya Karimjee kuaga mwili wa aliyekuwa Mkurugenzi wa Magonjwa yasiyopewa Kipaumbele katika Shirika la Afya Duniani (WHO), Dkt. Mwele Malecela aliyefariki nchini Uswizi mwishoni mwa wiki iliyopita.

Mwili wa Dk. Mwele umewasili usiku wa kuamkia leo Februari 19, 2022 kutokea Geneva ambako umauti ulimkuta.

Akizungumza wakati wa kutoa salam za pole, Rais Mwinyi amesema; “Kwa muda wote ambao nimemfahamu Dkt. Mwele, kikazi alikuwa ni mtu wa kujituma sana ‘committed and very professional.


“Dkt. Mwele ameitumikia Nchi yake, sisi sote tunapaswa tujiulize endapo tutaweza kufikia yale ambayo ameyafikia na ukiacha upande wa kazi kama mtu alikuwa na utu mkubwa, alikuwa karibu sana na watu alikuwa anapenda kusaidia, amesema Mwinyi.

Kwa upande wake, Waziri Mkuu Majaliwa amesema; “Nimekuja kutoa salamu za Rais
Samia Suluhu ambaye angependa kujumuika hapa kutoa pole amenituma nilete salamu za pole kwa familia kufuatia kifo cha mpendwa wetu Dkt. Mwele, amesema atakaporudi atakuja kukusalimia mzee Malecelam, amesema Majaliwa.

Baada ya kuagwa Karimjee, Mwili wa Dk. Mwele utasafirishwa kwenda nyumbani kwao Dodoma kwa ajili ya maziko.



Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments