MISS MAREKANI AJIUA KWA KUJIRUSHA GHOROFANI




Cheslie Kryst (30) aliyekuwa mlimbwende wa Marekani mwaka 2019 amefariki dunia. Kwa mujibu wa Polisi, Cheslie alijirusha ghorofani jana Jumapili, Januari 30, 2022 majira ya asubuhi huko Manhattan, New York.

Kabla ya kujirusha aliweka bandiko la picha yake Instagram yenye ujumbe; “Siku hii ikuletee Pumziko la Amani” ambapo familia yake imethibitisha kutokea kwa kifo hicho. Cheslie alikuwa na Shahada mbili ikiwemo ya Sheria na Shahada ya Uzamili ya Usimamizi wa Biashara.

“Ni huzuni na mafadhaiko makubwa ambayo familia tumeyapata kutokana na msiba wa mpendwa wetu Cheslie, alikuwa mwema na mwenye ushawishi duniani kote hasa kwa urembo na umaridadi wake.

“Cheslie alikuwa na upendo wa dhati, kwa kutumia uwezo wake na ushawishi wake amewasaidiwa wengi hasa katika kazi zake za uanasheria ikiwemo kuhakikisha wanyonge wanapata haki zao. Lakini cha ziada alikuwa binti yetu, dada, rafiki, mwenzetu na mshauri pia,” imesema familia yake.


Kryst, alikuwa wakili wa mahakama ya Division I na North Carolina, alishinda taji la Miss USA, Mei, 2019, na kushiriki katika Mashindano ya Miss Universe mwaka huo huo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments