WAZIRI MKUU : HATUNA MGONJWA WA OMICRON


Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa, ameitaka sekta binafsi kuitetea nchi kwa kuwa vita ya kibishara ni kubwa ikiwemo baadi ya watu kuitangaza Tanzania kuwa ni moja ya nchi hatari za kutembelea kwa madai ya kwamba wimbi la nne la kirusi cha Omicron limeshaingia.

Kauli hiyo ameitoa hii leo Desemba 11, 2021, jijini Dar es Salaam, wakati wa kongamano la biashara na uwekezaji.

"Juzi hapa mmesikia tena, Tanzania ni nchi hatarishi kwa ugonjwa mpya wa wimbi la nne, sisi hatuna mgonjwa hata mmoja wa wimbi la nne hospitali, yote hiyo ni vita ya kibiashara kwahiyo sekta binafsi mtusaidie kusema haya, tukiacha watu wanapotosha wanaharibu nchi," amesema Waziri Mkuu

Chanzo - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments