MSUKUMA ATOA NENO WANAOBEZA PhD YAKE



Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Musukuma


Mbunge wa Geita Vijijini, Joseph Kasheku maarufu kama Musukuma, amesema kwamba kuhusu watu wanaobeza PhD yake mitandaoni atalizungumzia jambo hilo kuanzia Ijumaa.

Kauli hiyo ameitoa hii leo Desemba 8, 2021, kwenye kipindi cha Supa Breakfast cha East Africa Radio, alipoulizwa analipi la kusema baada ya watu wengi kumbeza tangu atunukiwe udaktari wa heshima katika siasa na uongozi kutoka Chuo cha Academy of Universal Global Peace cha Marekani.

"Bahati mbaya mimi siko mitandaoni na kuhusu wanaonibeza, mimi nitazungumza kuanzia Ijumaa, sasa hivi bado nasoma tu hayo mambo yao wanayoyaandika," amesema Musukuma.
 
Chanzo - EATV

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments