HUYU NDIYE RAIS MWENYE UMRI MDOGO ZAIDI..GABRIEL BORIC WA CHILE



Gabriel Boric ameahidi mageuzi makubwa ili kukabiliana na ukosefu wa usawa wa kiuchumi nchini Chile

Mgombea wa mrengo wa kushoto Gabriel Boric ameshinda uchaguzi wa urais nchini Chile na kuwa kiongozi mwenye umri mdogo zaidi kuwahi kutokea nchini humo.


Katika kile kilichotarajiwa kuwa kinyang'anyiro kikali, kiongozi huyo wa zamani wa waandamanaji mwenye umri wa miaka 35 alimshinda mpinzani wake wa mrengo mkali wa kulia José Antonio Kast kwa pointi 10.

Bw Boric aliwaambia wafuasi wake kuwa atajali demokrasia, na kuahidi mageuzi katika mfumo wa uchumi wa Chile.


Ataongoza nchi ambayo imetikiswa katika miaka ya hivi karibuni na maandamano makubwa ya kupinga ukosefu wa usawa na ufisadi.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments