ZARI THE BOSS LADY ASHINDA TUZO MBILI


MJARISIAMALI kutoka Uganda mwenye makazi yake huko nchini Afrika ya Kusini Zarinah Hassan maarufu ‘Zari the boss lady” ameshinda tuzo mbili za 2021 African Social Entertainment Awards (ASEA) Nchini Afrika kusini.

Zari amejinyakulia tuzo ya mjasiriamali Bora wa mwaka pamoja na tuzo ya Mwanamke wa kisasa wa mwaka ‘sophisticated woman of year’.

Kupitia kurasa zake za mitandao ya kijamii, Zari ambaye ni mama wa watoto watano, alitoa shukrani za dhati kwa mashabiki wake kwa kumfanya kuibuka mshindi kwenye tuzo hizo.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments