Tanzia : ASKOFU PROF. RANWELL MWENISONGOLE AFARIKI DUNIA


CITY Christian Church (C.C.C) -TAG Upanga jijini Dar es Salaam limempoteza shujaa wa injili,Askofu Mkuu Mstaafu wa Awamu ya Pili na Mchungaji Kiongozi wa TAG Upanga,Profesa Ranwell Mwenisongole.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Mwinjilisti Dkt. Magnus Mhiche,Kaimu Katibu Mkuu na Makamu Askofu Mkuu wa TAG  Desemba 25,2021 imethibitisha kutokea kwa kifo hicho.


"Wapendwa watumishi wa Bwana kwa masikitiko makubwa Ofisi Kuu TAG Makao Makuu Dodoma inawataarifu msiba uliotupata wa kuondokewa na shujaa wetu Askofu Mkuu Mstaafu wa Awamu ya Pili na Mchungaji Kiongozi wa TAG Upanga Rev Dr Ranwell Mwenisongole.


"Shujaa amerudi nyumbani.Mungu aifariji familia na kanisa kwa ujumla katika kipindi hiki kigumu cha majonzi.Taarifa zingine zaidi mtajulishwa baadae.Bwana ametoa na Bwana ametwa jina lake libarikiwe,"ameeleza.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments