RASMI XAVI KOCHA MPYA BARCELONA


************************** 

NA EMMANUEL MBATILO 

Kiungo wa zamani Barcelona na timu ya taifa ya Hispania Xavi Hernandez amejiunga rasmi na klabu hiyo kama kocha mkuu mara baada ya kutimuliwa kwa aliyekuwa kocha Mkuu wa klabu hiyo Ronald Koeman. 

Nyota huyo ambaye alicheza kwa mafanikio katika klabu hiyo ametambulishwa leo mbele ya waandishi wa habari na kupokelewa na mashabiki waliojitokeza kwenye dimba la Camp New. 

Amesema amekuja katika klabu ambayo imemlea na kumtambulisha kwenye soka hivyo kuwa kocha katika klabu hiyo atahakikisha anapambana kurudisha mambo yalivyokuwa zamani.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments