MESSI ANYAKUA TUZO YA BALLON D'OR 2021



*************************

NA EMMANUEL MBATILO

Mchezaji wa klabu ya PSG ya nchini Ufaransa na timu ya taifa ya Argentina Lionel Messi amefanikiwa kunyakua tuzo ya Ballon D'or kwa mwaka 2021 mbele ya mpinzani wake Robert Lewandowski ambaye ameibuka mshindi wa pili kwenye kinyang'anyiro hicho.

Wachezaji watano ambao waliiongia kwenye tano bora ni Lionel Messi(PSG), Ngolo Kante (Chelsea), Jorginho (Chelsea),Robert Lewandowski (Bayan Munich) na Karim Benzema (Real Madrid).

Messi amefanikiwa kuchukua tuzo hiyo mara saba kwake na kumuacha Christian Ronaldo ambaye amechukua tuzo hiyo mara tano.

Tuzo ya klabu bora ya mwaka imeenda kwa timu ya Chelsea ambayo imekjuwa na wachezaji wengi walioingia kwenye kinyang'anyiro ya tuzo ya Ballon D'OR.

Tuzo hizo zimetolewa leo usiku Novemba 29,2021 nchini Ufaransa.

Download/Pakua/Install App ya Malunde 1 blog Google Playstore Bofya Hapa

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia malundekadama@yahoo.com au WhatsaApp: + 255 757 478 553 au 0625 918 527

0/Post a Comment/Comments